KALAPINA AONGEA KUHUSU UJIO WA RICK ROSS


Nguli wa  Hip hop hapa  Bongo, lijulikanalo kama  Kikosi cha Mizinga lenye maskani yake  pande za  Kinondoni jijini Dar, Kalama  Masoud Kalapina amesema  ujio wa  nyota wa muziki huo kutoka Marekani Rick Ross kwenye tamasha  la Fiesta  2012 ni zaidi ya  shoo kwa  wasanii wa  Tanzania.
Akizungumza  na blog hii  mapema leo Kalapina amesema kuwa  wasanii wa Bongo hawataakiwi kwenda  kwenye shoo ya  fiesta  kwa ajili ya kupiga picha na mkali huyo kwa ajili ya facebook na twitter  ama kwenda kugusa  tumbo kwani hazitawasaidia chochote kwenye muziki wao.
Hatutakiwi kwenda kwa ajiri ya facebook na twitter isipokuwa  tunatakiwa  kwenda kujifunza mbinu anazotumia kutawala jukwaa na pia kujaribu kuzungumza naye kuhusu njia ambazo anatumia  kupata mafanikio kimuziki na zaidi  kipi kimemfanya  kuwa mmoja ya mastaa walioleta mapinduzi kwenye muziki wa sasa  alisema Kalapina.
Akiendelea  zaidi Kalapina  alisema  kuwa  ujio wa Ross ni kitu  kikubwa sana  kwenye muziki wetu wa Tanzania na kutasaidia kwa kiasi kikubwa  kuitangaza  nchi yetu  hivyo anatoa  pongezi zote kwa  kampuni ya  Clouds Media kwa  kufanikisha  ujio huu.

Comments

Popular posts from this blog