Posts

Showing posts from September 21, 2012
Image
WASAMARIA WEMA WAANZA KUMCHANGIA MTOTO JULIANA Mtoto Juliana Mwinuka mkazi wa Ludewa ambaye anahitaji msaada wa kutibiwa kutokana na tatizo la kuungua moto linalomsumbua . Hawa hapa chini ndio ambao wameanza kuguswa na tatizo la mtoto huyo kwa kuchangia fedha kwa njia ya M-PESA kwa namba 0754 026299  ama Tigo Pesa 0712 750199 Hashimu Mbambo (Tsh. 5,000), Neema Ayoub (Tsh 15,000),Onesmo Lulandala(Tsh 10,000),Gasto Mgeni (Tsh. 20,000)na Allin Allin (Tsh 10,000) na Mussa Ayoub (Tsh 10,000)mmiliki wa mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kwa niaba ya watanzania wote napenda kuwapongeza wote walioguswa na tatizo la mtoto Julian Mwinuka na kuwaomba wengine zaidi kujitokeza kuchangia chochote kwa namba hiyo hapo juu
Image
MBUNGE WA VITI MAALUMU IRINGA RITHA KABATI AMJIBU MSIGWA Mbunge wa viti maalumu Iringa kupitia CCM Ritha Kabati leo ameongea na wanahabari Iringa kwa kile anachodai kudhalilishwa na mbunge wa Iringa mjini kupitia tiketi ya CHADEMA Peter Msigwa. Kabati ameeleza kuwa mbunge huyo amekuwa siku ta tarehe 19 septemba katika mkutano wake uliofanyika katika eneo la soko kuu na kumtaka aelewe kuwa yeye ni mbunge wa kuteuliwa ambae pia ni mbunge halali ambaye anaweza kufanya kazi kwa uhuru na kwamba nayonafasi kubwa katika halmashauri ya mkoa na kueleza “Nimekuwa  nikichukizwa na tabia ya mbunge huyo kutopenda yeye kutumia nafasi aliyonayo katika kutoa hoja zainazohusu jimbo la Iringa bungeni kitu ambacho hanitendei haki”. Alisema Pia amemuomba msigwa kuiga mfano wa wabunge wengine katika meneo mengine na kuwa na ushirikiano kwa kuacha tofauti zao kwaajili ya maendeleo ya wananchi wa Iringa na kwa Tanzania kwa ujumla.   Hata hivyo ametaka wanasiasa kuacha malumbano i...
Image
MUDA WA MECHI ZA ‘LIVE’ SUPER WEEKEND. TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Septemba 21, 2012 Mechi tano za Ligi Kuu ya Vodacom za Super Weekend katika mzunguko wa kwanza zitakazooneshwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha Super Sport zitaanza kati ya saa 1-.30 jioni na saa 1 kamili usiku.   Septemba 28 mwaka huu kutakuwa na mechi kati ya Azam na JKT Ruvu itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 1 kamili usiku. Mechi ya Simba na Tanzania Prisons itakayochezwa Septemba 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itaanza saa 11 kamili jioni.   Yanga na African Lyon zenyewe zitapambana Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni wakati Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar zitaoneshana kazi Oktoba 1 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.   Mechi ya mwisho katika Super Weekend itakuwa Oktoba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikiwakutanisha wat...
Image
HOTELI YA PETER SAFARI's YA MBEYA KUISHITAKI YANGA. TAARIFA YA UONGOZI WA HOTEL YA PETER SAFARI’s KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSIANA NA MADAI YALIYOTOLEWA NA KOCHA WA TIMU YA YANGA BAADA YA KUMALIZIKA MCHEZO WAKE NA TANZANIA PRISON TAREHE SEPT 15, 2012. Karibuni katika mkutano mfupi ambao unalenga kuzungumzia  ama kuelezea masikitiko makubwa dhidi ya Kocha wa Timu ya Yanga TOM SAINTFIET aliyoyatoa kwa vyombo vya habari kuidhalilisha hoteli  yangu   juu ya huduma zake na kiwango chake alichokiita cha huduma  mbovu!. Kimsingi management ya  Peter safari’s Hotel na Uongozi wa chama cha wamiliki wa Mahotel Mkoa wa Mbeya, tumesoma na kusikiliza kwa masikitiko makubwa lawama zilizotolewa na Kocha huyo kuwa “hajawahi kulala kwenye hoteli ya hadhi ya chini kama hii  katika nchi 20 alizowahi kufanya kazi katika nchi za Afrika”. Uongozi wa hotel  na chama cha wamiliki wa hotel kwa u...
Image
YANGA kimenuka! Mwesigwa, Sendeu watimuliwa kazi. Sanga akizungumza na Waandishi wa Habari mida hi. kulia ni Tito Osoro, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na kushoto Isaac Chanji, Mjumbe wa kuteuliwa UONGOZI wa klabu ya Yanga ya Dar es Salaam, umeisimamisha kazi Sekretarieti nzima ya klabu, akiwemo Katibu Celestine Mwesigwa na Ofisa Habari, Louis Sendeu, kutokana na kile ilichoeleza utendaji usioridhisha. Akizungumza na Waandishi wa Habari ‘mida  hii’ makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga alisema kwamba maamuzi hayo yamefuatia kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika tangu saa 5:30 leo hadi saa 9:30. Wengine wanaokumbwa na panga hilo ni Masoud Saad, aliyekuwa Ofisa Utawala, Philip Chifuka aliyekuwa Mhasibu na Hafidh Saleh aliyekuwa Meneja ambaye anahamishiwa kwenye majukumu mengine.  “Tumesitisha mikataba ya sekretarieti nzima, pia tumefanya marekebisho, tumemtoa Meneja wa timu na muda si mrefu tutamtang...