MAMA KIKWETE AWAASA WALIMU NA WAZAZI KUSIMAMIA WATOTO VYEMA KATIKA ELIMU Na Anna Nkinda- Maelezo, Lindi Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) wilaya ya Lindi mjini Mama Salma Kikwete amewataka wazazi na walimu kushirikiana kwa pamoja na kuhakikisha wanafunzi wanakwenda shule na kusoma jambo ambalo litasaidia kupanda kwa kiwango cha elimu mkoani humo. Mama Kikwete ambaye pia ni Mke wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete alitoa rai hiyo hivi karibuni wakati akiongea na wananchi pamoja na wanafunzi wa kijiji cha Ruaha waliofika kumsalimia mara baada ya kumaliza mkutano wake na viongozi wa Halmashauri kuu ya tawi la Ruaha lililopo katika kata ya Mingoyo wilaya ya Lindi mjini. Mjumbe huyo wa Halmashauri Kuu Taifa alisema kiwango cha elimu katika mkoa huo kiko chini lakini kama wazazi watahakikisha watoto wao wanaenda shule kwa wakati na walimu wakihakikisha watoto wamefika shule na kuwafundisha kiw...