Ngorongoro Heroes waahidi ushindi 04/04/2014 | Posted by Akidajr | Michezo | 0 comments | 55 views NAHODHA wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20 ‘Ngorongoro Heroes’, Aishi Manula, amesema wamejipanga kwa ajili ya kupata ushindi kwenye mechi dhidi ya Kenya itakayochezwa mji wa Machakos, Jumapili. Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhiwa bendera timu hiyo katika ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), jana, Manula ambaye pia anaidakia Azam FC, alisema lengo lao ni kufanya vizuri kwenye mechi hiyo. Naibu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juliana Yasoda, akikabidhi bendera ya taifa, aliwataka wachezaji hao kujituma na kutanguliza uzalendo mbele bila kusahau kuwa mchezo wa mpira wa miguu ni ushirikiano. Alisema Tanzania ina wachezaji wengi wenye vipaji, hivyo waliop...