MBUNGE WA VITI MAALUMU IRINGA RITHA KABATI AMJIBU MSIGWA

Mbunge wa viti maalumu Iringa kupitia CCM Ritha Kabati leo ameongea na wanahabari Iringa kwa kile anachodai kudhalilishwa na mbunge wa Iringa mjini kupitia tiketi ya CHADEMA Peter Msigwa.
Kabati ameeleza kuwa mbunge huyo amekuwa siku ta tarehe 19 septemba katika mkutano wake uliofanyika katika eneo la soko kuu na kumtaka aelewe kuwa yeye ni mbunge wa kuteuliwa ambae pia ni mbunge halali ambaye anaweza kufanya kazi kwa uhuru na kwamba nayonafasi kubwa katika halmashauri ya mkoa na kueleza
“Nimekuwa  nikichukizwa na tabia ya mbunge huyo kutopenda yeye kutumia nafasi aliyonayo katika kutoa hoja zainazohusu jimbo la Iringa bungeni kitu ambacho hanitendei haki”. Alisema
Pia amemuomba msigwa kuiga mfano wa wabunge wengine katika meneo mengine na kuwa na ushirikiano kwa kuacha tofauti zao kwaajili ya maendeleo ya wananchi wa Iringa na kwa Tanzania kwa ujumla.
  Hata hivyo ametaka wanasiasa kuacha malumbano ili waweze kufanya kazi kwa vitendo na sio kutumia maneno ambayo hayana tija yoyote katika maendeleo ya nchi. Aliongeza kuwa anategemea muda wa kulumbana katika majukwaa ya kisiasa haujafika kwahiyo lengo kubwa ni kuondoa tofauti zilizopo ili kuleta maendeleo na kuwatendea haki wananchi wa Iringa mjini.

Comments

Popular posts from this blog