Tuhuma nyengine za rushwa Afrika Kusini.
Shirika linaloendesha treni za
kasi za Afrika Kusini, Gautrain, limekanusha taarifa za magazeti
zinazotuhumu kuwa kandarasi ilipatikana baada ya kulipa dola milioni-35.

Inaarifiwa kuwa kampuni husika na mfanya biashara huyo, wamethibitisha kuwa fedha hizo zililipwa, lakini walisema hayo ni malipo ya wakala.
Treni za Gautrain zilikusudiwa kusafirisha abiria kutoka uwanja wa ndege wa Johannesburg hadi kati ya mji huo, na mji wa Pretoria.
Umoja wa vyama vya upinzani, Democratic Alliance, umetaka kufanywe uchunguzi juu ya kandarasi hiyo.
Comments
Post a Comment